I'M TAZGENIUS MFALME WA DAWA TIBA ASILI TANZANIA



MAANA YA NYOTA:
Nyota inawakilisha kipawa, hatma ya mtu, lengo lililomfanya Mungu akulete hapa duniani na kusudi lako la maisha. Hivyo tunaposema nyota yako ipo au imechukuliwa maana yake hayo mambo yamechukuliwa au yapo. Kimsingi hakuna mtu asiye na maana tangu kuzaliwa kwake, kwasababu kila mtu aliye duniani amekuja kwa kusudi lake.
Kuna tofauti kati ya elimu na nyota; elimu sio nyota lakini elimu yaweza kunoa nyota. Na si kwamba kujifunza kunaleta nyota bali nyota ipo kwa wote lakini elimu inainoa nyota; na ndio maana ni rahisi kumwona mtu hana elimu lakini anamafanikio mahali fulani.
🖐KAZI YA NYOTA:
✨️️ Nyota humfanya mtu kuwa mahiri katika utendaji kazi wake. (Effectiveness)
✨️Nyota huleta ubunifu katika maisha ya kila siku (Creativity)
✨️Nyota inamfanya mtu anatenda kwa ufanisi (Efficiency)
✨️Nyota huleta mvuto kwa watu kutoka mbali ili kuleta vitu kwa ajili yako. (Attraction)
✨️Nyota humfanya mtu awe na maisha yenye mwelekeo na kibali mbele za watu(Acceptance and Favor)
✨️Nyota humfanya mtu kusikilizwa katika jamii.
🖐NYOTA ILIYOCHUKULIWA/ ILIYOFUNIKWA KICHAWI:
✨️Nyota ikifunikwa au kuchukuliwa kichawi maana yake mvuto, umahiri, ufanisi na uwezo unakuwa umechukuliwa au umefunikwa. Na ndio maana kuna watu wanahangaika kuanzisha kampuni, kujenga nyumba, kulima, au kufanya biashara kama nyota imefunikwa au kuchukuliwa kichawi huwezi kupokea mafanikio ya sahihi kwenye maisha. Watu wengi wanahangaika kuonekana au kukubalika lakini kumbe tatizo lipo kwenye nyota yaani imefunikwa au imechukuliwa kichawi.
✨️Wachawi wanaweza kuona nyota ya mtu na kuifunika ili isionekane; na kwa namna hii watu wengi wanaonekana hawana mafanikio katika maisha kumbe nyota zao zimefunikwa. Hivyo ni muhimu kupambana Kwa Jina la Yesu ili nyota yako ionekane.
🖐DALILI ZA NYOTA ILIYOFUNIKWA:.
✨️maisha kukosa mwelekeo; mtu akikosa nyota hata kama akiwa na elimu kama nyota haipo lazima mtu huyo atakosa mwelekeo.
✨️kukwama kibiashara na kuishi maisha kwenye madeni.
✨️Unafanya kazi lakini hupati maendeleo. Yaani mtu anapata mshahara mzuri lakini anakosa mafanikio halisi kwasababu ya nyota iliyofunikwa au kuibiwa.
✨️Wewe ni kiongozi lakini jamii haikutambui.
✨️Ukichangia hoja za mijadala mbalimbali hakuna anayekusikiliza.
✨️Umesoma lakini hupati kazi, na ukipata kazi haiendani na elimu yako
Maisha ya upweke na hakuna anayekujali katika familia.
✨️Unatenda kazi kwa bidii lakini hupandi cheo.
✨️Kama ni binti sifa zote lakini hakuna anayekuchumbia maana huonekani.
✨️Kuandamwa na mabalaa na mikosi.
✨️Kupotelewa na watu wa muhimu